HII ni historia ya kweli ya maisha yangu, kuna baadhi ya watu
nakutana nao wananiuliza kama hii ni hadithi kama ambazo nimekuwa
nikiandika magazetini. Nataka nisisitize kwamba hii ni historia ya kweli
kabisa ya maisha yangu, najaribu kuyapitia maisha yangu ya nyuma na
kuwaandikia watu kule nilikopitia.
Lengo langu ni nini? Kumtia moyo mtu aliyevunjika moyo na
kumfanya aamini inawezekana kufanikiwa hata kama unatoka familia
masikini. Nayasema haya kwa sababu wako watu leo hii wamekata tamaa
kabisa na kuamini kwamba watu fulani wanaweza kufanya vizuri maishani na
si wao, uongo mkubwa na mbinu ya shetani kuwafanya watu waendelee
kuteseka.
Yeyote anayesoma historia yangu ni lazima hata kama yuko
katika hali ngumu kiasi gani, aamini kwamba inawezekana, kama
iliwezekana kwangu inashindikanaje kwa mtu mwingine? Inuka hapo ulipo,
amini akili yako, fanya jambo jema hata kama ni dogo kiasi gani,
ukilifanya kwa muda mrefu hatimaye jambo kubwa litakutokea, huu kwangu
ni ukweli uliothibitishwa na mimi mwenyewe.
Lengo si kujitapa bali kuwaonesha watu jinsi Mungu anavyoweza
kumbariki mtu na ninajua kutoka ndani ya moyo wangu ya kwamba Mungu
alininyanyua kwa kusudi moja tu; yeyote aliyekata tamaa atakaponiangalia
mimi apate tumaini na kuamini kwamba kumbe inawezekana.
Endelea mwenyewe...
Kitu kimoja naomba niseme hapa ni kwamba kipindi chote wakati
namuuguza kaka yangu, baba, mama na ndugu zangu wote walikuwepo jijini
Dar es Salaam, wakiungana nami kwa kila jambo, familia yetu ilikuwa ya
umoja kupindukia hilo ndilo jambo Mungu alilotujalia. Hivyo baada ya
msiba, taarifa zilishasambaa kwa watu wote wa karibu.
Msiba huu wa kaka uliniumiza mno sikuwahi kuumia kiasi hicho maishani
mwangu pengine niseme ulinifanya nikumbuke mema yote ya nyuma
aliyonifanyia, aliipenda sana familia alikuwa tayari kuteseka kwa kitu
kidogo alichopata lakini aifanye familia yake iishi, hakika alikuwa mtu
muhimu mno, ni huyu ndiye aliyenipa mtaji ambao umenifikisha hapa nilipo
leo, Mungu amlaze mahali pema peponi.
Ni hapo ndipo msemo huu wa Kifo kisikie kwa jirani yako kikija kwako
kinauma mno uliingia ndani ya kichwa changu, nikauamini kwa jinsi
nilivyoumia, pamoja na yote nilikumbuka maneno ya baba kwamba huwa
wanaume hawalii hivyo nilijikaza kiume.
Watu walipofika nyumbani kunipa pole tuliongea mengi lakini ndani ya
moyo wangu nilikuwa na maumivu makali mno, yalipozidi sana niliingia
chumba na kulia. Ni mke wangu pekee aliyefahamu jambo hili na
kunibembeleza akinipa moyo na kunifariji na baada ya kutulia nilinawa
uso nikavalia miwani yangu ya rangi nyeusi kisha kutoka nje kuendelea na
mazungumzo na wageni wetu.
Mipango ya mazishi ikaanza, taarifa
zikapelekwa Nyakato ambako ndiko nyumbani kwetu. Mwenyekiti wa mtaa,
mzee Machota, vijana wote wa Mecco akina Matiku, Isdori na wengineo
wengi waliungana nasi mara baada ya kuwasili mjini Mwanza.
Ni kama vile msiba ulianza upya, walikuwepo ndugu wengi mno
kutufariji na kuomboleza pamoja nasi, naikumbuka kwaya moja ya AICC
Neema. Kwaya hii iliimba mno nyimbo za kututia nguvu, uchungu ukapungua
kidogo na utaratibu wa mazishi ukaanza.
Watu walikuwa wengi kupindukia, ni hapo ndipo nilipogundua upendo wa
watu wa Mwanza, nikagundua kwamba watu hao walinipenda kupita kiasi na
walinithamini na kunipa nguvu kwa mambo yote.
Baada ya ibada kwisha tulianza safari ya kwenda makaburini, nakumbuka
yalikuwa makaburi ya Kangae, hapo ndipo alipozikwa kaka yangu mpendwa,
Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi. Amina. Hakika nitamkumbuka
daima kwa wema wa ajali aliniotendea.
Wakati ibada inaendelea nikatupa macho yangu pembeni na kushuhudia
makaburi mengi madogo madogo yakiwa hapo, akili yangu ikarejea nyuma na
kumkumbuka dada yangu mpendwa Jesca ambaye alikufa miaka mingi
iliyopita, huyu alizikwa na kaburi lake kupotea kwa sababu ya umasikini
mkubwa tuliokuwa nao mimi na familia yangu, hivyo mahali alipozikwa
wakaja watu wenye fedha na kununua eneo lile kisha kuchimba na kujenga
nyumba za kifahari, kitu kilichopoteza kabisa kumbukumbu yake, moyo
wangu ukaniuma tena.
Nikaangua kilio bila kujali tena kwamba mimi kama kaka mkubwa wa
familia nilitakiwa kujikaza, hakika uvumilivu wangu ulishakwisha,
nikajikuta nikimwaga machozi mpaka rafiki zangu waliokuwa wamenizunguka
wakanisihi na kunibembeleza kwamba sikutakiwa kufanya hivyo hata kama
nilikuwa katika maumivu makali kiasi gani. Nadhani ni kwa sababu
hawakujua nini kinanisumbua ndani ya kichwa changu.
Wakati ibada inaendelea mimi niliwaza jambo moja tu, kununua shamba
ambalo niliamini lingeweza kuweka kumbukumbu nzuri kwa kizazi kijacho,
watoto na wajukuu wa watoto wetu, nikaapa kununua shamba kubwa ili
jambo lililokuwa limejitokeza kwa Jesca lisije likajirudia tena katika
familia yangu.
Nikatamani familia yangu iwe na shamba kwa ajili ya
kuzika ili kuweka historia kwa kizazi kijacho na kitakachodumu siku
zote, ibada ikawa imekwisha lakini ndani ya kichwa changu nikiwa na
wazo moja tu, kununua shamba. Sikutaka yaliyotokea kwa marehemu dada
yangu Jesca yatokee tena katika familia yangu hivyo ndivyo
nilivyojiapiza.
Ibada ikawa imekwisha na watu wakaanza kutembea kurejea tena
nyumbani kuendelea na shughuli nyingine nakumbuka nilipiga hatua moja na
niliponyanyua kupiga ya pili, nikageuka nyuma na kuangalia kaburi la
kaka yangu, nikalia kwa uchungu, tulikuwa tukiondoka na kumwacha peke
yake tena sehemu ambayo hapakuwa na mtu yeyote isipokuwa yeye tu.
Uchungu ulizidi zaidi pale nilipomwangalia mtoto mdogo wa kiume wa
kaka yangu ambaye aliachwa na mama yake. Hapo ndipo nilipojua nini maana
ya maisha lakini nikamuahidi Mungu kufanya kila kinachowezekana kumpa
mtoto huyo furaha maisha yake yote nikichukua jukumu lote la kumlea na
kumtunza vyema kama ambavyo baba yake alifanya kwangu.
Nikalia tena lakini nikatamka ndani ya moyo wangu kwamba hatimaye
shujaa alikuwa amepumzika baada ya kuteseka kwa muda mrefu, kufa kwa
kaka yangu kukanifanya mimi nichukue mikoba yote aliyokuwa nayo, jukumu
la kuitunza familia likarejea kwangu kwa mila na desturi za Kisukuma
mwanaume hata kama ni mdogo kiasi gani aliitwa kaka, hivyo ndivyo
ilivyo.
Tukarejea nyumbani na kuendelea kuomboleza, watu bado wakiwa nasi,
wakiendelea kutufariji na kututaka badala ya kuendelea kuhuzunika sasa
tufurahi na kumshukuru Mungu kwani ndiye anayepanga yote yatokee.
Siku zikaendelea kusonga mbele, mpaka siku ya tatu, watu wengi wakiwa
bado wapo nyumbani kwetu kutufariji, wanakwaya nao bado walikuwepo,
hawakuchoka kuwa nasi. Ninawashukuru sana na Mungu aendelee kuwabariki
siku zote.
Baadaye watu walianza kutawanyika kurejea makwao baada ya kukaa nasi
kwa kipindi kirefu, sasa ulikuwa wakati wa wao kuendelea na shughuli zao
na kutuacha sisi tufanye yetu kama familia. Hapa ni kama vile uchungu
ulirejea tena upya lakini kwa sababu ya majukumu hatukuwa na sababu ya
kuendelea kuwazuia, tukawashukuru na kuwatakia baraka zote huku
wakiahidi kuendelea kuwa nasi katika maombi.
Mimi pia na familia yangu baada ya kuhakikisha kila kitu kimekwenda
sawa tulianza mipango ya kurejea jijini Dar es Salaam ili kuendelea na
shughuli nyingine.
Usikose kufuatilia katika Gazeti la Ijumaa Wikienda wiki ijayo
Jumanne, 10 Juni 2014
HADITHI YA KUSISIMUA AISEEEEEE
BAADA ya gari kusimama pembeni na kutakiwa
watawa wote waliokuwa kwenye gari kushuka, Sister Anna alipinga kitendo
cha kushushwa kwenye gari.
“Jamani hivi watumishi wa Mungu wanaweza kuwa wauaji?”
“Sister hili ni agizo la mheshimiwa rais kuwakagua wote wanaopita njia hii, hasa baada ya mtuhumiwa kuonekana bonde la Kizugo. Sehemu yote ya mapori kumetanda wanajeshi kwa hiyo kila atakapokimbilia lazima ashikwe.”
“Sasa sisi tunahusika vipi na mtu huyo?”
“Sister we wasiwasi wako…
“Jamani hivi watumishi wa Mungu wanaweza kuwa wauaji?”
“Sister hili ni agizo la mheshimiwa rais kuwakagua wote wanaopita njia hii, hasa baada ya mtuhumiwa kuonekana bonde la Kizugo. Sehemu yote ya mapori kumetanda wanajeshi kwa hiyo kila atakapokimbilia lazima ashikwe.”
“Sasa sisi tunahusika vipi na mtu huyo?”
“Sister we wasiwasi wako…

Added by GLOBAL on June 9, 2014 at 8:00am —
9 Comments
A Saint and a Ghost (Mtakatifu na Mzimu) - 94
Mfululizo wa matukio ya ajabu
unaendelea kuyatawala maisha ya msichana mdogo, ambaye maisha yake
yametawaliwa na usiri mkubwa. Kwa kumtazama, huwezi kugundua chochote
kilichojificha nyuma ya maisha yake kwani uzuri wa sura yake, upole na
urembo wake, vinamfanya aonekane hana hatia machoni mwa watu.
Hata hivyo, kuna siri kubwa iliyojificha nyuma ya maisha yake ambayo ameishi nayo kwa kipindi kirefu. Ukweli ambao hakuna anayeujua ni kwamba msichana…
Hata hivyo, kuna siri kubwa iliyojificha nyuma ya maisha yake ambayo ameishi nayo kwa kipindi kirefu. Ukweli ambao hakuna anayeujua ni kwamba msichana…

Added by GLOBAL on June 9, 2014 at 7:00am —
7 Comments
True Memories Of My Life [Kumbukumbu za Kweli za Maisha Ya Shigongo] - 82
HII ni historia ya kweli ya maisha
yangu, kuna baadhi ya watu nakutana nao wananiuliza kama hii ni hadithi
kama ambazo nimekuwa nikiandika magazetini. Nataka nisisitize kwamba hii
ni historia ya kweli kabisa ya maisha yangu, najaribu kuyapitia maisha
yangu ya nyuma na kuwaandikia watu kule nilikopitia.
Lengo langu ni nini? Kumtia moyo mtu aliyevunjika moyo na kumfanya aamini inawezekana kufanikiwa hata kama unatoka familia masikini. Nayasema haya kwa sababu…
Lengo langu ni nini? Kumtia moyo mtu aliyevunjika moyo na kumfanya aamini inawezekana kufanikiwa hata kama unatoka familia masikini. Nayasema haya kwa sababu…

Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)